Tetesi tano kubwa jioni - Fastestsmm News Swahili
Chanzo cha picha, Getty Images
Imeripotiwa leo kuwa klabu ya Saudia Pro League, Al-Hilal imetuma ofa ya pauni milioni 25 kwa Fulham kwa ajili ya kumnunua mshambuliaji wa Serbia Aleksandar Mitrovic.
Vyanzo vya klabu vimemthibitishia Simon Stone wa Fastestsmm Sport kwamba ofa hiyo "imekataliwa" na "hawana hamu ya kumuuza" mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Serbia, ambaye alifunga mabao 14 Fulham iliporejea Ligi Kuu msimu uliopita, yuko chini ya kandarasi huko Craven Cottage hadi msimu wa joto wa 2026.
Chanzo cha picha, Getty Images
Nice wanasema wanatarajia Aaron Ramsey kurejea katika klabu kwa ajili ya mazoezi ya kabla ya msimu mpya kwani mustakabali wa nahodha huyo wa Wales bado haujulikani.
Mkataba wa Ramsey huko Nice ulimalizika mwezi uliopita, lakini kuna maoni kwamba mechi zake 34 kwao msimu uliopita zilitosha kuanzisha kifungu cha kuongeza.
Bila uthibitisho wowote, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 amefanya mazungumzo na Cardiff City kuhusu uwezekano wa kurejea.
Chanzo cha picha, Getty Images
Mfuasi wa Fulham amepigwa marufuku kujihusisha na soka kwa miaka mitatu baada ya kukiri kosa la hadharani linalohusiana na kuimba nyimbo za chuki dhidi ya wapenzi wa jinsia moja .
Josiah Norman, 25, kutoka Brixton, alikiri hatia katika Mahakama ya Westminster kwa kosa lililotokea wakati Fulham ilipocheza na Chelsea kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mnamo Februari.
Chanzo cha picha, Getty Images
Beki wa pembeni wa Tottenham Ryan Sessegnon huenda akakosa kuanza kwa msimu wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kupata jeraha la misuli ya paja kwenye mazoezi ambayo yamehitaji kufanyiwa upasuaji.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ameondolewa kwenye ziara ya klabu hiyo ya kabla ya msimu mpya ya Australia, Thailand na Singapore.
Chanzo cha picha, Getty Images
Huku Fulham ikiwa klabu ya hivi punde zaidi ya Ligi Kuu ya Uingereza kuzuwia kumtaka mmoja wa wachezaji wao kutoka Saudi Pro League, kuna tetesi za uhamisho mwingine.
Taarifa zinazomhusisha Jordan Henderson wa Liverpool na kutaka kuungana na mchezaji mwenzake wa zamani wa Anfield Steven Gerrard, ambaye sasa ni kocha wa Al-Ettifaq, zinazidi kupamba moto.
Mail sasa inaripoti kwamba kiungo huyo wa kati wa England mwenye umri wa miaka 33, ambaye alirejea kwa mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya akiwa na Liverpool wiki hii, atafanya uamuzi ndani ya saa 48 zijazo baada ya kupewa mkataba wa miaka miwili, kukiwa na chaguo la kuongeza 12 zaidi.
Post a Comment
0Comments